9Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
10Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
11Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
12Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
13Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.