Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 9

Yohana 9:9-14

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Baadhi yao wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “La! Ila anafanana naye.” Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, “Ni mimi!”
10Basi, wakamwuliza, “Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?”
11Naye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu. Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona.”
12Wakamwuliza, “Yeye yuko wapi?” Naye akawajibu, “Mimi sijui!”
13Kisha wakampeleka huyo mtu aliyekuwa kipofu kwa Mafarisayo.
14Siku hiyo Yesu alipofanya tope na kumfumbua macho mtu huyo, ilikuwa siku ya Sabato.

Read Yohana 9Yohana 9
Compare Yohana 9:9-14Yohana 9:9-14