Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 8

Yohana 8:44-51

Help us?
Click on verse(s) to share them!
44Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
45Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
46Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
47Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
48Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
49Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
50Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
51Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.”

Read Yohana 8Yohana 8
Compare Yohana 8:44-51Yohana 8:44-51