Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 8

Yohana 8:27-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
27Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
28Basi, Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
29Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”
30Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
31Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
32Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
33Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
34Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.

Read Yohana 8Yohana 8
Compare Yohana 8:27-34Yohana 8:27-34