Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 7

Yohana 7:37-49

Help us?
Click on verse(s) to share them!
37Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
38Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
39Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
40Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
41Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
42Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
43Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
44Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
45Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
46Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
47Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
48Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
49Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”

Read Yohana 7Yohana 7
Compare Yohana 7:37-49Yohana 7:37-49