Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 7

Yohana 7:20-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
20Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
21Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?

Read Yohana 7Yohana 7
Compare Yohana 7:20-25Yohana 7:20-25