Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 6

Yohana 6:46-55

Help us?
Click on verse(s) to share them!
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48Mimi ni mkate wa uzima.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

Read Yohana 6Yohana 6
Compare Yohana 6:46-55Yohana 6:46-55