Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 6

Yohana 6:33-40

Help us?
Click on verse(s) to share them!
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima.”
34Basi, wakamwambia, “Mheshimiwa, tupe daima mkate huo.”
35Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho.”

Read Yohana 6Yohana 6
Compare Yohana 6:33-40Yohana 6:33-40