Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 6

Yohana 6:28-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
28Wao wakamwuliza, “Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?”
29Yesu akawajibu, “Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma.”
30Hapo wakamwambia, “Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni.”
32Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima.”
34Basi, wakamwambia, “Mheshimiwa, tupe daima mkate huo.”
35Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.

Read Yohana 6Yohana 6
Compare Yohana 6:28-35Yohana 6:28-35