Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 5

Yohana 5:40-47

Help us?
Click on verse(s) to share them!
40Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
41“Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
42Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
43Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea.
44Mwawezaje kuamini, hali ninyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu ninyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?
45Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye ninyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.
46Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia; maana Mose aliandika juu yangu.
47Lakini hamuyaamini yale aliyoandika, mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?”

Read Yohana 5Yohana 5
Compare Yohana 5:40-47Yohana 5:40-47