Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 5

Yohana 5:29-40

Help us?
Click on verse(s) to share them!
29nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
30Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
31Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
32Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
33Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
34Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
35Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
36Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
37Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na
40hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.

Read Yohana 5Yohana 5
Compare Yohana 5:29-40Yohana 5:29-40