Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 4

Yohana 4:12-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.”
15Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”

Read Yohana 4Yohana 4
Compare Yohana 4:12-18Yohana 4:12-18