Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 3

Yohana 3:29-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
29Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika.
30Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
31Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
32Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
33Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
34Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
35Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.

Read Yohana 3Yohana 3
Compare Yohana 3:29-35Yohana 3:29-35