Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 3

Yohana 3:27-34

Help us?
Click on verse(s) to share them!
27Yohane akawaambia, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
28Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
29Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
30Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
31“Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
32Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
33Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
34Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.

Read Yohana 3Yohana 3
Compare Yohana 3:27-34Yohana 3:27-34