Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 20

Yohana 20:8-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.

Read Yohana 20Yohana 20
Compare Yohana 20:8-12Yohana 20:8-12