Text copied!
CopyCompare
Biblia Takatifu - Yohana - Yohana 20

Yohana 20:3-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,

Read Yohana 20Yohana 20
Compare Yohana 20:3-11Yohana 20:3-11