Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi

Zaburi 33

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Furahini katika Yahwe, ninyi wenye haki; kusifu kwa wenye haki kwa faa sana.
2Mshukuruni Bwana kwa kinubi; mwimbieni sifa kwa kinubi chenye nyuzi kumi.
3Mwimbieni yeye wimbo mpaya; pigeni kwa ustadi na muimbe kwa furaha.
4Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
5Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
6Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
7Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
8Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
9Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.
10Yahwe huvunja muungano wa mataifa; naye huishinda mipango ya wanadamu.
11Mipango ya Yahwe husimama milele, mipango ya moyo wake ni kwa ajili ya vizazi vyote.
12Limebarikiwa taifa ambalo Mungu wao ni Yahwe, watu ambao yeye amewachagua kama warithi wake.
13Yahwe anatazama kutoka mbinguni; yeye huona watu wote.
14Kutokea mahali ambapo yeye anaishi, huwatazama wote waishio juu ya nchi.
15Yeye anaye iumba mioyo yao na kuyaona matendo yao yote.
16Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa; shujaa haokolewi na nguvu zake nyingi.
17Farasi sio salama kwa ajili ya ushindi; ijapokuwa nguvu zake ni nyingi, hawezi kuokoa.
18Tazama, macho ya Yahwe yako kwa wale wanao mhofu yeye, wale wanao litumainia agano lake takatifu

19kuwaokoa maisha yao na mauti na kuwaweka hai wakati wa jaa.
20Sisi tunamngoja Yahwe, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21Mioyo yetu hufurahia ndani yake, kwa kuwa tunaamini katika jina lake takatifu.
22Yahwe, agano lako takatifu, liwe pamoja nasi tuwekapo tumaini letu katika wewe.