Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Nehemia

Nehemia 7

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Wakati ukuta ulipomalizika na milango nimekwisha kuisimamisha, na walinzi wa malango na waimbaji na Walawi walikuwa wamechaguliwa,
2nikampa ndugu yangu Hanani kuwa na amri juu ya Yerusalemu, pamoja na Hanania ambaye alikuwa msimamizi wa kijiji, kwa kuwa alikuwa mwaminifu na alimuogopa Mungu zaidi kuliko wengi.
3Nami nikawaambia, Msifungue malango ya Yerusalemu mpaka jua litakapokuwa kali. Wakati walinzi wa mlango wanalinda, unaweza kufunga milango na kuikaza. Chagua walinzi kutoka kwa wale wanaoishi Yerusalemu, wengine mahali pa kituo chao cha ulinzi, na wengine mbele ya nyumba zao wenyewe.
4Sasa jiji lilikuwa pana na kubwa, lakini kulikuwa na watu wachache ndani yake, na hakuna nyumba zilizojengwa tena.
5Mungu wangu aliweka moyoni mwangu, kuwakusanya pamoja wakuu, maafisa, na watu kuwaandikisha katika familia zao. Nilipata Kitabu cha kizazi cha wale ambao walirudi kwanza na nikaona kwamba imeandikwa humo.
6Hawa ndio watu wa jimbo ambao walikwenda kutoka kwenye uhamisho wa wale waliohamishwa ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwachukua mateka. Wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenda kwenye mji wake.
7Walikuja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana. Idadi ya wana wa Israeli ilikuwa.
8Wana wa Paroshi, 2, 172.
9Wana wa Shefatia, 372.
10Wana wa Ara, 652.
11Wana wa Pahath Moabu,
12kwa wana wa Yeshua na Yoabu, 2, 818.
13Wana wa Elamu, 1, 254.
14Wana wa Zatu, 845. Wana wa Zakai, 760.
15Wana wa Binnui, 648.
16Wana wa Bebai, 628.
17Wana wa Azgadi, 2, 322.
18Wana wa Adonikamu, 667.

19Wana wa Bigwai, 2, 067.
20Wana wa Adini, 655.
21Wana wa Ateri, wa Hezekia, 98.
22Wana wa Hashumu, 328.
23Wana wa Besai, 324.
24Wana wa Harifu, 112.
25Wana wa Gibeoni, 95.
26Watu kutoka Bethlehemu na Netofa, 188.
27Watu wa Anathothi, 128.
28Watu wa Beth Azmaweth, 42.
29Watu wa Kiriath Yearimu, Kefira, na Beerothi, 743.
30Watu wa Rama na Geba, 621.
31Watu wa Mikmasi, 122.
32Watu wa Betheli na Ai, 123.
33Watu wa Nebo, 52.
34Watu wa Elamu wa pili, 1, 254.
35Watu wa Harimu, 320.
36Watu wa Yeriko, 345.

37Watu wa Lodi, Hadidi, na Ono, 721.
38Watu wa Senaa, 3, 930.
39makuhani Wana wa Yedaya (wa nyumba ya Yeshua), 973.
40Wana wa Imeri, 1, 052.
41Wana wa Pashuri, 1, 247.
42Wana wa Harimu, 1, 017.
43Walawi, wana wa Yeshua, wa Kadmieli, wa Binui, wa Hodavia, 74.
44Waimbaji wana wa Asafu; 148.
45Waliofungua mlango wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni; wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai, 138.
46Watumishi wa Hekalu wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi,
47wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni,
48wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai,
49wana wa wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari.
50Wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda,
51wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea,
52wana wa Besai, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu.
53Wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri,
54wana wa Baslith, wana wa Mehida, wana wa Harsha,

55wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema,
56wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
57Wana wa Sulemani, wana wa Sotai, wana wa Sofeereth, wana wa Peruda,
58wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli,
59wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokerethi Sebaimu, wana wa Amoni.
60Watumishi wote wa hekalu, na wana wa watumishi wa Sulemani, walikuwa 392.
61Hawa ndio watu waliokwenda kutoka Tel Mela, Tel harsha, Kerub, Addon, na Imeri. Lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba wao au jamaa za baba zao walikuwa wana wa Israeli,
62wana wa Delaya, wana wa Tobia, na wana wa Nekoda, 642.
63Na kutoka kwa makuhani Wana wa Habaya, Hakosi, na Barzilai (akamchukua mkewe kutoka kwa binti za Barzilai wa Gileadi na akaitwa kwa jina lao).
64Hawa walitafuta rekodi zao kati ya waliojiunga na kizazi chao, lakini hawakuweza kupatikana, kwa hivyo waliondolewa katika ukuhani kama walio najisi.
65Naye mkuu wa gavana akawaambia wasiruhusiwe kula chakula cha makuhani kutoka kwenye dhabihu mpaka atakapoinuka kuhani mwenye Urimu na Thumimu.
66Kusanyiko lote lilikuwa 42, 360,
67isipokuwa watumishi wao wa kiume na watumishi wao wa kike, ambao walikuwa 7, 337. Walikuwa na wanaume na wanawake wa kuimba 245.
68Farasi zao zilikuwa 736 kwa idadi, nyumbu zao, 245,
69ngamia zao, 435, na punda zao, 6, 720.
70Baadhi ya wakuu wa familia za baba zao walitoa zawadi kwa ajili ya kazi. Gavana alitoa sadaka ya darkoni elfu ya dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 ya makuhani.
71Baadhi ya wakuu wa familia za baba zao waliwapa katika hazina kwa kazi darkroni elfu ishirini za dhahabu na mane 2, 200 za fedha.
72Watu wengine waliwapa darkoni za dhahabu ishirini elfu, na dhahabu elfu mbili za fedha, na mavazi sitini na saba kwa makuhani.

73Basi makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, watu wengine, watumishi wa hekalu, na Israeli wote waliishi katika miji yao. Hata mwezi wa saba watu wa Israeli walikuwa wakiishi katika miji yao.”