Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 5

Mithali 5:4-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4lakini mwishoni anakuwa mchungu kama mnyoo, hukata kama upunga mkali.
5Miguu yake huelekea mauti; hatua zake huelekea njia yote ya kuzimu.
6Hafikirii njia ya uzima. Hatua za miguu yake hupotea, maana hajui anakwenda wapi.
7Sasa, wanangu, nisikilizeni; wala msiache kusikiliza maneno ya kinywa changu.
8Lindeni njia yenu mbali naye wala msiende karibu na mlango wa nyumba yake.
9Kwa njia hiyo hamtawapa wengine heshima yenu au miaka ya uzima wenu kwa mtu mkatiri;
10wageni usije kufanya karamu kwa utajiri wenu; kazi mliyoifanya haitaenda katika nyumba ya wageni.
11Mwishoni mwa maisha yenu mtajuta ambapo nyama na mwili wenu vitaangamia.
12Nanyi mtasema, “Namna gani nilichukia fundisho na moyo wangu ulidharau sahihisho!
13Sikuweza kuwatii walimu wangu au kuwasikiliza walionielekeza.

Read Mithali 5Mithali 5
Compare Mithali 5:4-13Mithali 5:4-13