6usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.