Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 4

Mithali 4:4-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
5Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
6usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.

Read Mithali 4Mithali 4
Compare Mithali 4:4-11Mithali 4:4-11