Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 4

Mithali 4:16-24

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
17Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
18Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
19Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
20Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
21Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
22Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
23Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
24Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.

Read Mithali 4Mithali 4
Compare Mithali 4:16-24Mithali 4:16-24