Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 4

Mithali 4:12-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
13Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
15Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
16Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
17Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
18Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
19Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
20Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
21Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.

Read Mithali 4Mithali 4
Compare Mithali 4:12-21Mithali 4:12-21