6Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.