Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 30

Mithali 30:21-31

Help us?
Click on verse(s) to share them!
21Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara:
25mchwa ni viumbe ambao sio imara, lakini huandaa chakula chao wakati wa hari,
26Wibari siyo viumbe wenye nguvu, lakini hutengeneza makazi yake kwenye miamba.
27Nzige hawana mfalme, lakini wote wanamwendo wa mpangilio.
28Kama mjusi, unaweza kumkunja kwa mikono yako miwili, lakini wanapatikana katika majumba ya wafalme.
29Kuna vitu vitatu ambavyo ni fahari katika mwendo na vinne ambavyo ni fahari katika namna ya kutembea:
30simba, aliyeimara miongoni mwa wanyama- wala hajiepushi na kitu chochote;
31jogoo anayetembea kwa mikogo; mbuzi; na mfalme ambaye askari wapo kando yake.

Read Mithali 30Mithali 30
Compare Mithali 30:21-31Mithali 30:21-31