Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 30

Mithali 30:2-31

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Hakika nipo kama mnyama kuliko mwanadamu na sina ufahamu wa wanadamu.
3Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya Mtakatifu.
4Je ni nani amekwenda juu mbinguni na kurudi chini? Je ni nani aliyekusanya upepo kwenye mikono yake? Je ni nani aliyekusanya maji kwenye kanzu? Je ni nani aliyeziimarisha ncha za dunia yote? Jina lake ni nani, na jina la mtoto wake ni nani? Hakika unajua!
5Kila neno la Mungu limejaribiwa, yeye ni ngao kwa wale wanaokimbilia kwake.
6Usiyaongezee maneno haya, au atakukemea, na utathibitishwa kuwa mwongo.
7Vitu viwili ninakuomba, usivikatalie kwangu kabla sijafa:
8Majivuno na uongo viweke mbali nami. Usinipe umasikini wala utajiri, nipe tu chakula ninachohitaji.
9Maana nikipata vingi zaidi, nitakukana wewe na kusema, “Yehova ni nani?” Au kama nitakuwa masikini, nitaiba na kukufuru jina la Mungu wangu.
10Usimkashifu mtumwa mbele ya bwana wake, au atakulaani na utapata hatia.
11Kizazi ambacho kinachomlaa baba yao na hakimbariki mama yao,
12kizazi hicho ni safi katika macho yao wenyewe, lakini hawajaoshwa uchafu wao.
13Hicho ni kizazi- jinsi gani macho yao yanakiburi na kope zao zimeinuka juu! -
14kuna kizazi ambacho meno yao ni upanga, na mifupa ya taya zao ni visu, ili waweze kumrarua masikini wamtoe duniani na mhitaji atoke miongoni mwa wanadamu.
15Ruba anamabinti wawili, “Toa na Toa” wanalia. Kuna vitu vitatu ambavyo havitosheki, vinne ambavyo havisememi, “Inatosha”:
16Kuzimu, tumbo tasa, nchi yenye kiu kwa maji, na moto usiosema, “Inatosha.”
17Jicho ambalo linamdhihaki baba na kudharau utii kwa mama, macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni, na ataliwa na tai.
18Kuna vitu vitatu ambavyo vinanishangaza, vinne ambavyo sivifahamu:
19njia ya tai angani; njia ya nyoka juu ya mwamba; njia ya meli kwenye moyo wa bahari; na njia ya mtu pamoja mwanake kijana.
20Hii ni njia ya mzinzi- anakula na kufuta kinywa chake na kusema, “sijafanya ubaya wowote.”
21Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara:
25mchwa ni viumbe ambao sio imara, lakini huandaa chakula chao wakati wa hari,
26Wibari siyo viumbe wenye nguvu, lakini hutengeneza makazi yake kwenye miamba.
27Nzige hawana mfalme, lakini wote wanamwendo wa mpangilio.
28Kama mjusi, unaweza kumkunja kwa mikono yako miwili, lakini wanapatikana katika majumba ya wafalme.
29Kuna vitu vitatu ambavyo ni fahari katika mwendo na vinne ambavyo ni fahari katika namna ya kutembea:
30simba, aliyeimara miongoni mwa wanyama- wala hajiepushi na kitu chochote;
31jogoo anayetembea kwa mikogo; mbuzi; na mfalme ambaye askari wapo kando yake.

Read Mithali 30Mithali 30
Compare Mithali 30:2-31Mithali 30:2-31