Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 2

Mithali 2:10-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
12Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
13Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
14Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
15Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.
16Busara na hekima zitakuokoa kutoka kwa mwanamke malaya, kutoka kwa mwanamke anayetafuta visa na mwenye maneno ya kubembeleza.
17Yeye humwacha mwenzi wa ujana wake na kusahau agano la Mungu wake.
18Maana nyumba yake huinama na kufa na mapito yake yatakupeleka kwa wale walioko kaburini.
19Wote waiendeao njia yake hawatarudi tena na wala hawataziona njia za uzima.
20kwa hiyo utatembea katika njia ya watu wema na kufuata njia za wale watendao mema.

Read Mithali 2Mithali 2
Compare Mithali 2:10-20Mithali 2:10-20