Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 29

Mithali 29:4-26

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
5Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
6Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
7Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
8Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
21Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
22Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
23Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
24Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
25Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
26Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.

Read Mithali 29Mithali 29
Compare Mithali 29:4-26Mithali 29:4-26