Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 27

Mithali 27:13-24

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka.
21Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?

Read Mithali 27Mithali 27
Compare Mithali 27:13-24Mithali 27:13-24