Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 26

Mithali 26:5-14

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.

Read Mithali 26Mithali 26
Compare Mithali 26:5-14Mithali 26:5-14