Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 25

Mithali 25:19-28

Help us?
Click on verse(s) to share them!
19Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.

Read Mithali 25Mithali 25
Compare Mithali 25:19-28Mithali 25:19-28