Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 24

Mithali 24:16-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”

Read Mithali 24Mithali 24
Compare Mithali 24:16-29Mithali 24:16-29