Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 23

Mithali 23:22-27

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.

Read Mithali 23Mithali 23
Compare Mithali 23:22-27Mithali 23:22-27