Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 23

Mithali 23:12-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
12Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu.
15Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.

Read Mithali 23Mithali 23
Compare Mithali 23:12-23Mithali 23:12-23