Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 23

Mithali 23:1-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.

Read Mithali 23Mithali 23
Compare Mithali 23:1-9Mithali 23:1-9