Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 22

Mithali 22:3-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.

Read Mithali 22Mithali 22
Compare Mithali 22:3-12Mithali 22:3-12