Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 22

Mithali 22:14-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.

Read Mithali 22Mithali 22
Compare Mithali 22:14-25Mithali 22:14-25