Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:8-19

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:8-19Mithali 21:8-19