Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:22-30

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:22-30Mithali 21:22-30