2Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.