Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:19-26

Help us?
Click on verse(s) to share them!
19Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:19-26Mithali 21:19-26