Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:17-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:17-22Mithali 21:17-22