Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 21

Mithali 21:14-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.

Read Mithali 21Mithali 21
Compare Mithali 21:14-25Mithali 21:14-25