Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 20

Mithali 20:23-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
23Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.

Read Mithali 20Mithali 20
Compare Mithali 20:23-29Mithali 20:23-29