20Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?