Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 20

Mithali 20:13-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
13Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.

Read Mithali 20Mithali 20
Compare Mithali 20:13-29Mithali 20:13-29