Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 1

Mithali 1:8-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni.
13Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
14Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
15Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;

Read Mithali 1Mithali 1
Compare Mithali 1:8-15Mithali 1:8-15