Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 1

Mithali 1:22-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
22“Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
23Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
24Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
25Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
26Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
27hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
28Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
29Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,

Read Mithali 1Mithali 1
Compare Mithali 1:22-29Mithali 1:22-29