21Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.