Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Mithali - Mithali 18

Mithali 18:9-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
10Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
11Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
12Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
13Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
14Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
15Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
16Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
17Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
18Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.

Read Mithali 18Mithali 18
Compare Mithali 18:9-18Mithali 18:9-18